Jumapili, 23 Oktoba 2016

UNA TATIZO LA KISUKARI? HAPA PATA DAWA ZA ASILI NA NAMNA YA KUZIANDAA UKIWA KWAKO NYUMBANI 

 Dawa mbadala 10 zinazotibu Kisukari

 


1. UWATU

 

Tafiti nyingi zimeonyesha kuwa uwatu unao uwezo mkubwa katika kutibu kisukari. Uwatu huzisisimua seli katika kongosho kitendo kinachofanya uzalishwaji wa insulini kuongezeka. Maajabu haya ya uwatu yanasemekana kufanyika kutokana na uwatu kuwa na asidi amino mhimu sana ijulikanayo kama ‘4-hydroxyisoleucine’. Miaka mingi kabla hata ya huu utafiti kufanyika, uwatu umekuwa ukitumika kama moja ya dawa bora kabisa za asili katika kutibu kisukari.

Namna ya kuutumia Uwatu kujitibu kisukari

• Chota mbegu za uwatu vijiko 4 na uziloweke katika maji robo lita kwa usiku mmoja. Asubuhi ponda ponda hizo mbegu za uwatu ndani ya maji kisha zichuje na upate maji yake. Kunywa maji haya kila siku asubuhi kwa muda wa miezi 2.
• Chukuwa uwatu ya unga vijiko vikubwa 2 na uweke ndani ya maziwa au maji ya uvugu uvugu robo lita, koroga vizuri na unywe kila siku kutwa mara 2 kwa miezi 2.
• Chukuwa gramu 100 za mbegu za uwatu na gramu 50 za binzari manjano. Unaweza kuongeza kiasi kidogo cha pilipili manga nyeupe kwenye mchanganyiko huu. Ongeza kijiko 1 cha mchanganyiko huu wote katika maziwa robo lita na unywe kutwa mara 2 kila siku.
• Unaweza pia kuongeza uwatu ya unga katika unga wako unaotumia kutengenezea mkate au hata chapati.

2. MDALASINI

 

Utafiti uliofanywa kwa watu wenye kisukari aina ya pili umeonyesha kuwa utumiaji wa gramu 1 hadi 6 za mdalasini kwa siku unaweza siyo tu kupunguza kaisi cha damu sukari mwilini, bali pia unaweza kupunguza kiasi cha mafuta mazito katika damu (triglyceride) na hata kudhibiti kolesto!
Waathirika wa kisukari pia hutokewa kuwa na matatizo katika mfumo wao wa upumuwaji, hivyo utumiaji wa mdalasini kwao unaleta maana zaidi kwakuwa mdalasini unao uwezo mkubwa katika kuzuia magonjwa katika mfumo wa upumuwaji pia. Mdalasini ya unga hushusha kiwango cha damu sukari kwa kuziamsha shughuli za insulini. Mdalasini pia ina faida kwa watu waliogunduliwa kuwa na kisukari cha mwanzo (pre-diabetes status) na hivyo matumizi ya mdalasini kwao yatasaidia kuzuia wasipatwe na kisukari katika siku za usoni.
Hata hivyo aina ya mdalasini unaotumia pia inahusika katika kutibu kisukari au maradhi mengine. Nashindwa kupata maneno haya kwa Kiswahili lakini kuna aina kama mbili hivi za mdalasini ambazo ni ‘Cassia cinnamon’ ambao wenyewe huwa na kitu kingine ndani yake kiitwacho ‘coumarin’ ambayo ni sumu na husababisha matatizo katika ini. Mdalasini nzuri kwa kutibu kisukari na ambayo bei yake ipo juu kidogo ni ile iitwayo kwa kiingereza kama ‘Ceylon cinnamon’.

Namna ya kutumia mdalasini kutibu kisukari

• Chukuwa lita 1 ya maji na uyachemshe. Mara yatakapoanza kuchemka, ongeza vijiko 3 vikubwa vya mdalasini ya unga na uache kwa dakika kama 15 hivi kisha ipuwa chuja na unywe ikiwa bado ya uvugu uvugu kutwa mara moja kila siku kwa mwezi 1.
• Ongeza mdalasini kijiko kidogo kimoja cha chai katika kikombe kimoja (robo lita) cha maji ya uvugu uvugu, koroga na unywe kila siku.
• Unaweza pia kuongeza mdalasini ya unga ndani ya kachumbari kila unapokula.

3. MAJANI YA MANJANO

 

Utafiti unaonyesha kuwa, kutokana na kuwa na kiasi kingi cha madini kama vile madini ya chuma, Zinki, na shaba; majani ya manjano ni mhimu sana katika kuutunza usawa wa glukozi katika damu. Madini haya huziamsha seli za kongosho zinazohusika na uzarishwaji wa homoni ya insulini. Majani ya manjano pia husaidia umeng’enywaji wa wanga mwilini. Yanao uwezo wa kuviamsha upya vimeng’enya katika figo na ini ambazo zinahusika katika kumeng’enya wanga na kuurudisha katika hali yake ya kawaida na hivyo kusaidia kutibu kisukari.
Wagonjwa wa kisukari huwa wana tatizo la kuwa na uwezo mdogo kudhibiti sumu mwilini jambo ambalo hupelekea seli zao za mwili kufa katika kiwango kingi. Utafiti unaonyesha kuwa majani ya manjano yana uwezo wa kupunguza kiasi cha seli kufa, seli ambazo ni mhimu katika uzarishwaji wa insulini.
Majani ya manjano yanaweza kushusha usawa wa damu sukari na ni mhimu sana kwa watu wanaopata kisukari kama matokeo ya uzito kuzidi. Ikiwa kisukari kinazunguka katika familia yenu, jitahidini kutumia majani ya manjano kwakuwa yamethibitika kuthibiti pia hata kile kisukari cha kurithi.

Namna ya kutumia majani ya manjano kujitibu kisukari

• Tafuna majani freshi ya manjano 7 mpaka 10 kila siku asubuhi.
• Tumia majani ya manjano kwenye kila chakula unachopika kila siku.

4. MSHUBIRI (Aloe Vera) 

 

Wakati mshubiri umekuwa ukitumika kwa miaka mingi katika kutibu kisukari, baadhi ya tafiti za hivi karibuni zimeonyesha kuwa mshubiri unao uwezo pia katika kushusha kiwango cha damu sukari na mafuta katika mzunguko wa damu kwa wagonjwa wanaosumbuliwa na kisukari. Mshubiri umethibitika katika kutibu kisukari cha aina ya kwanza na hata cha aina ya pili.

Jinsi ya kuandaa mshubiri kutibu kisukari

Changanya vifuatavyo:
• Jeli ya mshubiri kijiko cha chai 1
• Unga wa majani ya matunda ya damu ya mzee kijiko cha chai 1
• Unga wa manjano kijiko cha chai 1
Kunywa mchanganyiko huu kila siku kabla ya chakula cha mchana na jioni

5. MAJANI YA MUEMBE

 

Wakati tunda la embe halina uwezo wa kutibu kisukari, majani ya mti wa muembe yanao uwezo huo! Waganga wengi wa Nigeria wamekuwa wakitumia sana majani ya muembe katika kutibu kisukari. Yanao uwezo wa kupunguza ufyonzwaji wa glukozi katika utumbo mkubwa hivyo kusaidia kupunguza usawa wa sukari katika damu. Pia yana uwezo mkubwa katika kudhibiti kiwango cha mafuta katika damu.

Namna ya kuandaa

• Loweka majani 10 mpaka 15 ndani ya nusu lita ya maji kwa usiku mmoja. Chuja maji haya asubuhi mapema na uyanywe kabla ya kula chochote. Subiri lisaa limoja lipite ndipo ule chakula cha asubuhi.
• Kausha majani ya muembe kwenye kivuli. Yatakapokuwa yamekauka kabisa, yasage kupata unga wake na hifadhi unga huu katika chombo kisafi na kisha lamba unga huu nusu kijiko kidogo cha chai kila siku kabla ya chakula cha mchana na jioni.

6. MREHANI

 

Mrehani (basil) una faida nyingi sana kiafya. Nje ya kudhibiti kisukari, Mrehani pia una sifa na uwezo katika kudhibiti asthma, kuondoa mfadhaiko, kudhibiti bakteria, kudhibiti virusi, kudhibiti vivimbe, kuondoa sumu mwilini, kudhibiti asidi tumboni, na kuongeza kinga ya mwili. Mrehani huzisaidia pia seli za kongosho kufanya kazi zake vizuri na kusaidia utolewaji au uzarishwaji mzuri wa insulini.
Jinsi ya kuutumia mrehani kutibu kisukari
• Tafuna majani mawili mpaka manne ya mrehani kila siku asubuhi kabla hujala chochote.
• Ponda majani ya mrehani kupata juisi yake kama kijiko kimoja hivi cha chai na unywe kila siku asubuhi kabla ya kula kitu chochote.


7. BAMIA

 

Bamia zina kiasi kingi cha vitamini A, B6, C, K, magnesium, potassium, zinki, na faiba. Bamia ina uwezo mkubwa katika kusawazisha usawa wa sukari mwilini. Mbegu za Bamia zina kidhibiti kiitwacho alpha-glucosidase ambacho huzuia wanga kujibadili kuwa glukozi. Faiba iliyomo kwenye bamia husaidia kurekebisha kiwango ambacho sukari humeng’enywa katika utumbo mkubwa.
Jinsi ya kutumia Bamia katika kujitibu Kisukari
Mahitaji:
• Bamia 2 mpaka 3
• Maji glasi 1
Jinsi ya kuandaa:
• Zisafishe bamia vizuri kabisa.
• Ondoa au ikate sehemu ya kichwa na mkia katika bamia na utupe. Kisha kata kila bamia katikati kwa urefu ili kupata vipande 2, hivyo utapata jumla vipande 4 kwa bamia hizo 2.
• Hivyo vipande 4 viweke ndani ya glasi iliyojaa maji, funika na uache hivyo kwa usiku mmoja.
• Asubuhi na mapema kunywa hayo maji yote yaliyokuwa na bamia kabla ya kula kitu kingine chochote. Ukiweza unaweza kula hata hizo bamia pia. Bamia mbichi zinafaida zaidi mwilini kuliko zilizopikwa.
• Fanya hivi kila siku kwa miezi kadhaa.

8. MBEGU ZA KATANI

 

Mbegu za katani zina kiasi kingi cha mafuta mhimu sana yajulikanayo kama “essential omega-3 fat alpha-linolenic acid (ALA)’’, pia zina protini, faiba na muunganiko wa mmea uitwao ‘lignans’. Hii lignans hufanya kazi kama kiuaji sumu au kwa maneno mengine hufanya kazi ya kuondoa sumu mwilini. Baadhi ya tafiti zimeonyesha kuwa mbegu za katani zinao uwezo wa kusawazisha usawa wa damu sukari mwilini kwa vile zina kiwango kikubwa cha faiba ndani yake. Mbegu za katani zinasaidia katika kazi za kumeng’enya chakula, pia husaidia katika ufyonzaji mzuri wa mafuta na sukari. Kama unatumia mara kwa mara hizi mbegu za katani, kiasi chako cha sukari chaweza kushuka hadi asilimia 28 kwa wakati mfupi.

Jinsi ya kutumia mbegu za katani katika kutibu kisukari

• Ongeza kijiko kikubwa kimoja cha unga wa mbegu za katani ndani ya glasi ya maji au maziwa na unywe wakati wa chakula chako cha asubuhi.
• Ongeza kijiko kidogo kimoja cha chai cha unga wa mbegu za katani katika nafaka zako unazotumia wakati wa chakula cha asubuhi.
• Ongeza pia unga wa mbegu za katani katika supu.

9. Chai ya Majani ya Mpapai

 

Majani ya mpapai ni mazuri katika kuongeza ufanisi wa insulini. Ni mazuri kwa watu wenye kisukari cha aina ya pili. Pia majani ya mpapai husaidia kupunguza matatizo yawezayo kuwatokea watu wenye kisukari, matatizo kama vile mafuta kwenye ini, matatizo katika kibofu cha mkojo na pia husaidia kupunguza mfadhaiko/stress. Kuna faida nyingine kubwa zaidi ya kutumia majani ya mpapai ambayo ni uwezo wake katika kutibu vidonda vitokanavyo na kisukari kwa haraka zaidi. Waganga wengi wa tiba asili kutoka Japani na Australia Na wengine wengi toka mataifa mbalimbali wamekuwa wakitumia majani ya mpapai kutibu kisukari kwa miaka mingi sasa.
Mahitaji:
• Majani 10 ya mpapai
• Maji lita 2

Maandalizi:

• Tumbukiza hayo majani ya mpapai katika maji.
• Chemsha hayo majani katika maji kwenye moto hadi maji yatakapobaki nusu yake (lita 1).
• Ipuwa na uache ipowe
MENGI ZAIDI ENDELEA KUTEMBELEA BLOGG HII
DAWA ZA ASILI JITIBU PRESHA YA KUPANDA NA KISUKARI KWA KUTUMIA TIBA HII YA ASILI : 

 Tiba inasaidia pia kuyeyusha mafuta yasiyo hitajika mwilini. 

Kinywaji  hiki  cha  ajabu  kitakusaidia  kushusha  presha, kuyeyusha  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini, kupambana  na  kisukari  na  kuimarisha  mfumo  wa  mmen’genyo  wa  chakula  katika  mwili  wako.
Mahitaji
    • Kijiko 1 kidogo  cha  mdalasini
    • Vijiko  viwili  vikubwa  vya  apple  cider  vinegar
    • Kijiko  kimoja  kikubwa  cha  asali  mbichi.
    • Vijiko  viwili  vikubwa  vya  juisi  ya  limao.
    • Glasi  moja  ya  maji
MATAYARISHO :
Weka   vitu  vyote  hivyo  kwenye  blender  na  usage  kwa  pamoja  kasha  uhifadhi  kwenye  chombo  kisafi  na  salama.
MATUMIZI
Kunywa  dawa  yako  kila  siku  asubuhi  kabla  haujatia  kitu  chochote  tumboni.
TENGENEZA   MCHANGANYIKO  WAKO  KILA  SIKU  KWA  SABABU  NI  RAHISI  KUTENGENEZA.
Matokeo  ya  kutumia  mchanganyiko  huu  yatakuwa  ya  kushangaza  na  kustaajabisha.
 DAWA ZA ASILI ZA KUTIBU MAGONJWA MBALIMBALI

 Tengeneza dawa za magonjwa mbalimbali ukiwa kwako nyumbani kupitia maelekezo yafuatayo......
Dawa hizi ni asili kabisa na hazina madhara kabisa

MAGONJWA NA JINSI YA KUYATIBU
(1)PUMU-
Matumizi;(a)hutibiwa kwa kutumia;simbi zaidi ya 20,ndimu nyingi na asali.Kunywa mchanganyiko huu kijiko 1 mara3 kwa siku hadi upone.AU kula vitunguu maji kwa wingi
(b)Pembe ya mbuzi-kausha kisha usage na unga wake changanya na asali na ulambe mara 3 kwa siku
(2)NGUVU ZA KIUME-
Hutibiwa kwa kutumia;
(a)kitunguu swaumu-
Matumizi;ponda na changanya na asali ya njano na ulambe asali hiyo kijiko1 mara3 kwa siku tumia mchanganyiko huu kwa wiki 2.
(b)tende na rose-
matumizi;changanya na maziwa na kisha kunywa wiki1-wiki3.
(c)mchele mkavu-
(d)Tikiti maji,tangawizi,pilipilinafaka halisi,mbogamboga za majani
Matumizi;tafuna mchele kidogo lisaa limoja kabla ya kujamiiana utarudiwa na nguvu zako.
KIFUA/KUKOHOA-
Hutibiwa kwa kutumia mchanganyiko wa;asali,kitunguu maji,kitunguu swaumu na tangawizi;
Matumizi;twanga mchanganyiko huu pamoja kisha ndio utumie.
(3)MAGONJWA YA MOYO-
Matumizi;kunywa juisi ya vitunguu maji kwa wingi.
(4)MAPAFU-
Matumizi;kula zabibu au kunywa juisi yake kwa wingi kila siku.
(5)GESI-
Matumizi;kunywa maji glasi8 au zaidi kwa siku.
(6)MAWE KATIKA KIBOFU CHA MKOJO-
Matumizi;kula chakula kilichopikwa na manjano.
(7)UVIMBE KATIKA SEHEMU ZA SIRI NYUMA-
Matumizi;paka alovera mahali penye uvimbe mara 3 kwa siku.
(8)KUPATA CHOO KIKUBWA-
Matumizi;kunyia chai ya tangawizi
(9)KICHOMI-
Matumizi;kula ndizi mbivu kila siku.
MAJIPU NA VIDONDA VISIVYOPONA-
Matumizi;binzari ya manjano koroga katika maji upate uji mzito kisha paka sehemu iliyoathirika mara2 kwa siku.AUchanganya zafarani kiasi na unga wa risasi na weka maziwa ya mbuzi kidogo kisha paka kwenye kidonda.
(10)MAUMIVU MAKALI TUMBONI-
Matumizi;changanya vijiko2 vya tangawizi na castro oil kisha kunywa mara 2 kwa siku.
(11)MIFUPA ILIYOVUNJIKA-
Matumizi;kula nusu nanasi kila siku hadi upone.AU kaanga vitunguu maji na uboho(rojorojo)
(12)MAUMIVU YA VIUNGO/MGONGO-
Vifaa;mafuta ya simsim,haba souda,na pilipili manga
Matumizi;chemsha,chuja na paka kwenye maeneo yanayouma yakiwa na uvuguvugu.
(13)KUTAPIKA DAMU-
Matumizi;weka kuzubara katika siki kali masaa24,ongeza sukari na chuja kisha unywe kutwa mara3
(14)KUSAGA CHAKULA NA KUIMARISHA TUMBO DHAIFU-
Vifaa;habasouda vijiko2, pilipili manga2,karafuu2
Matumizi;changanya kisha kunywa kijiko1 cha chai ndani ya kinywaji chochote cha uvuguvugu
(15)KIFUA/MARADHI-
Vifaa;juisi ya figili kikombe cha kahawa,kijiko kikubwa cha asali
Matumizi;changanya na maji ya moto kikombe cha chai yaache yapoe ndio unywe kutwa mara2 asubuhi na jioni.
(16)KIKOHOZI CHA MUDA MREFU-
Vifaa;khardal,asali safi ya nyuki.
(17)KUONDOA COLESTEROL-
Vifaa;tembe 3,kitunguu swaumu,kijiko1 cha zaatari,maji lita1
Matumizi;chemsha kidogo kunywa kikombe1 mara3 kwa siku.
(18)HIGH BLOOD PRESSURE/LOW BLOOD PRESSURE-
Vifaa;papai na tangawizi
Matumizi;sagapapai na tangawizi kamua juisi yake kunywa kutwa mara2 AU chemsha na kunywa juisi ya mmung'unya mara3 kwa siku
(19)KIKOJOZI-
Vifaa;ufuta mweusi na maziwa
Matumizi;saga ufuta mweusi na unga wake koroga kijiko1 ndani ya maziwa kunya mara2 kwa siku asubuhi na jioni mpaka upone
(20)HEDHI ILIYOKITHIRI/HEDHI KWA WINGI-
Matumizi;koroga unga wa ufuta mweusi ndani ya maji ya moto kisha kunywa AU chukua unga wa giligilani glasi1 chemsha katika nusu lita ya maji kisha kunywa nusu glasi mara3 kwa siku.
(21)KISUKARI-
Matumizi;chukua kijiko1 cha mdalasini weka katika kikombe cha kahawa kunywa kutwa mara3 kwa siku40 AU tengeneza juisi ya bitter gourd kunywa kila siku
(22)MAUMIVU YA MIGUU NA MAGOTI-
Matumizi;chukua kijiko1 kidogo cha zafarani changanya katika chai ya moto kunywa kutwa mara3
(23)KUZUIA MIMBA KUTOKA-
Matumizi;chukua kijiko 1 cha unga wa amla changanya na asali,kunywa kwa muda wa wiki1
(24)KUACHA SIGARA-
Matumizi;chukua hamira changanya vijiko 2 katika glasi1 ya maji na unywe pamoja na unga wake,kunywa glasi1 kutwa mara3
(25)KICHWA-
Matumizi;kula samaki na tangawizi
(26)KUVIMBIWA-
Matumizi;kula ndizi mbivu
(27)BARIDI YABISI-
Matumizi;kula tangawizi
(28)KIBOFU-
Matumizi;kula kunazi nyekundu
(29)BP-
Matumizi;zabibu nyeusi1kg,giligilani nusu,twanga kisha uchemshe na kunywa nusu glasi mara 3
(30)KWIKWI-
Matumizi;twanga hiliki changanya na maziwa kisha kunywa glasi moja
(31)DEGEDEGE-
Matumizi;ponda vitunguu swaumu kisha mpake  mwenye tatizo hilo na uichome na mfukizie
(32)UGONJWA WA KUSAHAU-
Matumizi;chukua zabibu kavu changanya na kungumanga na utafune mara2 kwa siku21
(33)MAWE KATIKA FIGO-
Matumizi;kitunguu maji chekundu,cheupe na njano,kata vipande4 kila kimoja weka vipande hivyo katika sufuria baada ya kuvisaga acha ichemke kisha kunywa jusi yake
(34)DAMU PUANI-
Vifaa;siki,limao,chumvi
matumizi;chukua chumvi kijiko kidogo weka katika glasi changanya na siki mpaka  chumvi iyeyuke ,kamulia limao nusu tumia siku3 mpaka 4 mfululizo 
TIBA MBADALA KWA KUTUMIA MBOGAMBOGA NA MATUNDA
(1)BOGA-Lina vitamini B kwa wingi
HUTIBU;
a.Huupa mwili nguvu
b.Huondoa tatizo la kufunga choo
c.Hurekebisha utolewaji wa nyongo mwilini
d.Huongeza nguvu za kiume
e.Husaidia kuvunja nguvu za sumu mwilini
f.Husaidia kupata mkojo hivyo kusafisha figo
g.Husaidia kuondoa mawe kwenye figo(Kidney stone)
h.Linafaa kwa wagonjwa wa kisukari
i.Husaidia kuimarisha glandi za kiume zitoazo mbegu za uzazi(PROSTATE GLAND
MAANDALIZI
-Chukua boga lililokomaa na katakata lisage kwenye blender(kama huna blender waweza kuliponda kwenye kinu safi na likishalainika ongeza maji kidogo kusudi upate juice yake.Wakati unakamua juice usiondoe mbegu na kiini.
NB.MAANDALIZI HAYA HUTEGEMEA UGONJWA UNAOTAKA KUUTIBU
(2)KAROTI-Ina vitamini nyingi mbalimbali
HUTIBU;
a.kulainisha tumbo
b.Inapigana na kutibu upungufu wa damu
c.Inasafisha damu
d.Inasaidia kutibu uvimbe wa saratani
e.Inatibu baridi yabisi
f.Inatibu chunusi,vidonda tumbo,koo,macho na kibofu
MAANDALIZI;
-Chukua karoti kilo1 ponda iwe laini na kisha uchemshe kwa dakika 15 ndani ya maji lita 1 na nusu au mbili chuja,kunywa juisi yake kwa kutibu vidonda tumbo au saratani ya tumbo,saratani ya kizazi tumia nusu kikombe cha chai miezi 3 mpaka 6,kwa kurembesha uso nawia juisi yake kila asubuhi mfululizo kwa siku 5.
(3)UNGA WA MKAA-
Unaweza kupata kupata kutoka kwenye mti wa mkuyu,kifuu cha nazi,msonobari au mkaratusi
INATIBU;
a.Kuumwa na nyoka
b.Kunywa sumu
c.Uvimbe
d.Kutapika,kiungulia,macho,kuharisha na kuhara damu ,kusaga chakula,vidonda tumbo,tindikali na kuungua
MAANDALIZI
a.Choma kifuu cha nazi hadi kiwe mkaa
b.Saga uwe unga(kwa miti tumia magome)
-Chukua kijiko 1 kikubwa cha unga na koroga katika maji safi ya kunywa ya vuguvugu kikombe 1 kunywa kabla ya kula kwa kutibu vidonda tumbo,kutoa asidi
KUUMWA NYOKA-
-Shona kifuko cha kitambaaa.
-Chota unga wa mkaa kijiko kikubwa na uweke ndani ya kifuko na tia maji kidogo na ufunge na nyingine ndani ya maji vuguvugu kikombe 1 uwe kama uji na umpe anywe kwa mtu aliyekunywa sumu tumia njia hiyo ya kunywa
MACHO-
-Weka katika kifuko kama hapo juu na ufunge kwenye jicho ,fanya hivyo kwa siku 3 mfululizo wakati wa usiku.
(4)GILIGILANI-
Inatibu tumbo,moyo na hedhi nk
MAANDALIZI
-Vijiko 2 vikubwa vya giligilani iliyosagwa ndani ya maji lita 1 kisha chemsha kwa dakika 10 na kunywa nusu kikombe kutwa mara 3 kwa siku 5 
(5)NYONYO-
-Majani yanatibu kifua kikuu na uvimbe wa miguu
-Mizizi ni dawa ya mafindofindo,macho ya njano,uvimbe,kisonono na kaswende
-Kikonyo chake ni dawa ya kwikwi-jaza maji ya baridi katika kikombe cha chai na kikonyo mpe mgonjwa anywe kila baada ya dakika 3 mpaka kwikwi iishe
-Kunywa punje yake na maji glasi kwa siku kwa muda wa siku 5 inatibu MOTODASI AU MOTO WA MUNGU
-Tumia majani kwa kupasha moto na kufungia miguu inayouma au kukandia miguu inayouma
-Kwa magonjwa ya zinaa kama kisonono na kaswende mizizi kiasi na chemsha ndani ya maji nusu lita kisha kunywa kikombe cha chai kutwa mara 3 kwa muda wa siku 5
(6)SWAUMU-
HUTIBU
a.Kuumwa kichwa
b.Kibofu cha mkojo
c.Matatizo katika damu,chunusi nk
d.Macho kutoona vizuri,pumu,figo,ukurutu(fungus),baridi yabisi,majipu nk
NAMNA YA KUITUMIA KUTIBU BAADHI YA MAGONJWA;
A.Shinikizo la damu:Tumia juisi ambayo waweza kuichanganya kwenye saladi kama chakula cha pembeni
MAANDALIZI
-Menya chengachenga za kitunguu swaumu zipatazo 10-30 na kuziponda na zikishalainika na kutoa maji kaua juisi yake na uweke kwenye chombo kisafi
-Chukua malimao 2 au 3 uyakamue upate juisi yake na ulichanganye na ile ya kitunguu swaumu na uiache usiku kucha na asubuhi koroga vizuri na anza kuitumia kwa kunywa kijiko 1 cha chai kila baada ya saa moja na hakikisha hukiachi kijiko hicho ndani ya juisi kwani hutengeneza sumu.Magonjwa ya kichwa pia hutibiwa kwa njia hii kama unataka kuitumia kutibu magonjwa kwa muda mrefu waweza kuichemsha na kuiweka katika chupa safi pindi inapopoa na utumie kikombe cha chai kila asubuhi na jioni na pia waweza kutumia saladi yake wakati wa chakula.
B.Ukurutu(fungus)-
-Twanga kitunguu swaumu na weka kwenye eneo lililoathirika na uifungie kwa bandeji na kuacha kwa nusu saa na endelea kufanya hivyo kwa muda wa wiki mbili hii ni pamoja na magonjwa ya ngozi
C.Vidonda mdomoni,mafindofindo,kuharisha,maumivu ya tumbo na kunyonga-
-Kwa matatizo mengine ya kifua kula kikonyo kimoja cha kitunguu swaumu kutwa mara tatu kulingana na ukubwa wa kitunguu.
(7)NANASI-
-Nanasi lina vitamini A,B,C pia lina madini ya chuma ,calcium, na copper ambayo ni muhimu kwenye mifupa,meno,neva na misuli(MUSCELS)
HUTIBU;
a.Matatizo mbalimbali ya tumbo,magonjwa ya bandama(SPILEN),ini,utumbo mwembamba,homa,magonjwa ya midomo(VIDONDA),magonjwa ya koo,ugonjwa wa kusahau,maradhi ya akili,hali ya kukosa mori(LOW SPIRIT)
b.Aidha nanasi huondoa matatizo ya wanawake ambayo husababishwa na upungufu wa shughuli za homoni au makosa fulani katika sehemu ya yai ,huondoa shida ya kufunga choo,baridi yabisi,upungufu wa damu(ANEMIA) na maambukizo kwenye maungio ya mifupa(ARTHRITIS).Aidha kwa kula au kunywa juisi ya nanasi husaidia akina mama wanaonyonyesha walio na maziwa kidogo na hata wale wajawazito wanashauriwa kutumia mananasi
-Pia ni kichocheo kizuri katika kupona haraka kwa mifupa iliyovunjika.
BIRINGANYA(EGGS PLANTS)-
-Tunda la biringanya ukilipika kama mboga linatibu vidonda tumbo na linasaidia kupata usingizi.Kwa wale wenye tatizo la kukosa usingizi (INSOMNIA)wanashauriwa kula biringanya kwa wingi.
-Biringanya huharakisha kupona magonjwa na kuleta afya nzuri mwilini.Ikumbukwe kuwa usingizi ni kitu muhimu sana kwa afya ya mwili wa binadamu na ustawi wake.
-Kwa kutumia tunda hili kama mboga katika mlo ulao husaidia kunenepesha kwa wale wanaotaka kunenepa.hakikisha katika mlo ulapo na ufurahie chakula unachokila kila siku ,tumia kwa muda wa mwezi mmoja utaona matokeo yake.
KWA USHAURI, MAONI,MASWALI NA TIBA wasiliana kupitia